1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages

 
 
 

 

Matukio ya Kisiasa | 29.11.2008

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kukutana tena na kiongozi wa waasi nchni Congo

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa leo amewasili Goma kwa mazungumzo na kiongozi wa waasi Laurent Nkunda katika jaribio la kukomesha mzozo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Olusegun Obasanjo ambaye alikuwa na mazungumzo na Rais Joseph Kabila mjini Kinshasa hapo jana alikuwa anatarajiwa kuondoka kwa helikopta kutoka Goma kuelekea kwenye eneo la Rutshuru linaloshikiliwa na waasi kwa ajili ya mkutano wake huo na Nkunda.Obasanjo amewaambia waandishi wa habari mjini Goma kwamba anataka kumueleza Nkunda juu ya kile kilichofanyika tokea akutane naye mara ya mwisho.

Rais huyo wa zamani wa Nigeria anaandamana na rais mwengine wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa ambaye anauwakilisha Umoja wa Afrika.Mkpa amasema anataka kumpima Nkunda ambaye anadai kuwahami Watutsi walio wachache mashariki mwa jimbo la Kivu Kaskazini.Amesema anataka kumsikiliza anafikiria nini juu ya kurudisha amani,utulivu na umoja nchini Congo.

Hapo jana Mkapa amekataa kuzungumzia kwa ukamilifu mazungumzo ya wajumbe hao na Kabila lakini amedokeza kwamba sio rahisi kwa Nkunda kutimiziwa adai lake la kukutana moja kwa moja na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

 

Mohamed Dahman

 
Share this article

Send us an e-mailSendPrint

More on the topic



 
Picture of the Day
ImageOfTheDay

DW-TV EUROPE live

Journal (deutsch) - Mit Tagesthema